![]() |
![]() |
![]() |
S.L.P 1219, Musoma - Tanzania Simu +255 28 2620920/2620255 , +255 784 582 786/555: taarifa@juasun.net [ In English ] |
![]() |
![]() |
|
Upatikanaji Kwa wakati huu huduma hii inapatikana maeneo ya Musoma Mjini,Bunda Mjini, Wilaya ya Pangani mkoani Tanga na Makao makuu ya Wilaya zilizo nje ya Miji ambako kampuni ya simu TTCL inahudumia. Vifaa vinavyohitajika Ili kuunganishwa na mtandao wa mawimbi, kompyuta yako itaunganishwa na kifaa cha redio na antenna, ambavyo vyote vitatolewa na Juasun.Net. Gharama Malipo ya awali yatapangwa kutegemea muda wa hitaji kama vile:- (a)Mambomba kwa ajili ya kufunga antenna. (b)Waya aina ya UTP/STP kiasi cha Tsh 1,200/= kwa mita. (c)Waya kwa ajili ya kinga ya radi itategemea urefu wa bomba. (d)Ardhi fimbo (Earth rod) 2 kila moja Tsh 3,500/=. (e)Vifaa vya ujenzi wa msingi pamoja na saruji Tsh 15,000/=. (f)Clips pakiti moja Tsh 3,500/=. (g)Waya kwa ajili ya kuimarisha nguzo ya bomba Tsh 3,500/=. (h)Gharama za kuunganishwa Tsh 30,000/= kwa kila Kompyuta. Malipo ya kila mwezi ni Tsh. 54,000/= kwa kila kompyuta na Tsh 24,000/= kama gharama za kukodi Antenna/CPE. Mteja mpya lazima awe na UPS kwa ajili ya kulinda vifaa kwa tatizo la umeme. Upatikanaji: Ni rahisi iwapo tu mteja ana huduma nzuri ya simu ya mezani (TTCL) Vifaa vinavyohitajika Utahitaji kuwa na kifaa kiitwacho modem ambacho wataalamu wetu watakiandaa ili kiweze kufanya kazi na mitambo ya Juasun.Net. Gharama Gharama za kuunganishwa ni Tsh.25,000/= (malipo yake hufanyika mara moja tu) Gharama kwa mwezi ni Tsh.26,000/= Upatikanaji Kwa wakati huu huduma hii hupatikana Wilaya za Bunda na Serengeti, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano kwa Maendeleo Vijijini (ICT4RD) majaribio. Iwapo umevutiwa na huduma zetu au unahitaji maelezo zaidi waweza kuwasiliana nasi kwa anuani zilizoko hapo juu |