Huduma
ya VoIP (Voice over Internet Protocol) Juasun.net
VoIP ni
nini?
VoIP- Hii ni huduma inayomuwezesha mtumiaji
wa kinakilishi kwa njia ya mtandao (Internet)kuwasiliana na
mtumiaji mwingine kwa kutumia mawimbi ya sauti (kufanya mazungumzo)
kama mazungumzo kwa njia ya simu.
Huduma
ya VoIP hutumikaje?
Huduma hii huunganishwa na mtandao wa internet moja kwa moja
na kumfanya mtumiaji aweze kupiga simu bure. Hii inafanya
urahisi kwa mtumiaji kufanya kazi ya ofisi akiwa nje ya ofisi,
nyumbani au mahali popote iwapo tu huduma hii ya VoIP inapatikana.
Huduma hii hutolewa
na kampuni ya mawasiliano kwa njia ya kinakilishi, Juasun.net
kwa wanachama wake wote na pia mtu yeyote anayependa kujiunga
na huduma hii kwa gharama ambazo mtumiaji anaweza kuzimudu.